habareeeee, mi napenda saana kula matunda yasiyo na ladha ili kuepusha
sukari isyo na tija mwilini. na tango ni moja ya matunda niyapendayo na tena
nilile bila kumenya ila liwe limeoshwa vizuuuri.
Leo tunaangalia faida za tango kiafya. kama kuna mtu hajawahi
kulila, kama yupo namshauri aanze leo.nikiwa na sababu za msingi kabisa nazo ni
hizi!Tango lina virutubisho vingi na madini muhimu sana katika mwili wa
binadamu. Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, miongoni mwa virutubisho na madini
mengine yaliyomo, tango ni chanzo kizuri cha Kashiamu (IRON), ama Chuma,
Phosforas, Potasiamu, Zinki, Kambalishe, Vitamini B complex, Vitamini C na
Vitamin E.
Unaweza kusema kuwa kirutubisho cha ‘Potasiamu’ ndiyo chakula cha moyo, kwa
sababu ‘potasiamu’ ndiyo inayouwezesha moyo kupiga mapigo yake ya kawaida na
kuustawisha. Ulaji wa matunda na vyakula vyenye kiwango kikubwa cha ‘potasiamu’
kama tango, ni muhumi sana kwa mtu mwenye matatizo ya moyo, presha ya kupanda
na matatizo ya mapigo ya moyo.
Aidha, tango linaaminika kupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini ,tango
huimarisha misuli ya mwili na bila kusahau husaidia usagaji wa chakula tumboni
hivyo kuondoa tatizo la ukosefu wa choo.
Virutubisho vilivyomo kwenye tango pia, hutoa afueni kwa mtu mwenye matatizo ya
ini, kongosho, figo na matatizo katika kibofu cha mkojo. Wataalamu wetu
wanatueleza pia kuwa tango lina kirutubisho kinachojulikana kama ‘erepsin’
ambacho husaidia uzalishaji wa ‘amino acids’ ambazo ni muhimu kwa uzalishaji wa
protini mwilini.
Vile vile, tango lina kiwango kingi cha Vitamin C, hivyo kuwa na uwezo mkubwa
wa kuondoa matatizo yatokanayo na ukosefu wa Vitamin C, kama vile kutokwa na
damu kwenye fizi, upungufu wa damu kwa watoto wachanga na kuota meno na mifupa
vibaya.
faida kubwa kuliko zote za kula tunda tango au juisi yake mara kwa
mara ni kinga dhidi ya saratani za aina mbalimbali. Jambo hili linatokana na
ukweli kwamba tango lina kiwango kikubwa cha (uchachu). Kwa kawaida
‘seli’ za saratani ‘haziwezi kuishi’ kwemye mazingira yenye uchachu, hivyo
tango kinga ni kinga dhidi ya saratani.
turejee zama za mababu kidogo, Tangu enzi na enzi, tango limekuwa likitumika
katika masuala ya urembo wa ngozi, watu wengi hutumia tango kwa njia mbalimbali
kutunza ngozi zao na kupendezesha sura zao. Hata baadhi ya vipodozi visivyo na
madhara, hutengenezwa kutokana na tango.
Ulaji wa tango na unywaji wa juisi yake mara kwa mara, huondoa matatizo mengi
ya ngozi yaliyomo ndani na nje ya mwili. Utakapotumia juisi ya tango kwa muda
wa wiki mbili hadi tatu mfululizo, utakuwa na ngozi nyororo na yenye afya
kushinda hata mtu anayetumia vipodozi.
kama unataka kujaribu kunywa juice ya tango kama nlivyokwambia , Ni rahisi
sana, chukua tango lako moja au zaidi, lioshe vizuri na limenye, kisha katakata
vipande tayari kwa kusaga, ama kwa mashine au kwa kutwanga kwenye kinu
maalum, changanya na maji safi kiasi ili kupata juisi kiasi cha glasi moja.
Unaweza kuweka sukari kiasi kidogo sana kisizidi kijiko kimoja kwa glasi
ili kupata ladha au weka asali kijiko kidogo kimoja. Utapata matokeo
mazuri na ya haraka kama ukinywa juisi yako kila siku asubuhi kabla ya kula
kitu chochote.
Ili kutibu matatizo ya ngozi uliyonayo au magonjwa mengine kama tulivyoyaeleza
hapo juu, kunywa juisi hiyo kwa muda wa wiki mbili hadi 4 mfululizo na angalia
matokeo yake. Kwa afya yako, weka mazoea ya kunywa japo mara mbili au
tatu kwa wiki juice ya tango.
Vile vile, unaweza kujiwekea mazoea ya kula tango kwa njia mbalimbali kama vile
kuchanganya na saladi, kachumbari au kutafuna lenyewe mara kwa mara, kwani
faida zake mwilini ni nyingi anza leo.