
Kutana na Regina Mwalekwa
Monday, June 23, 2014
MUNGU NI WA WOTE NA ANA MAJINA LUKUKI
Monday, February 18, 2013
ALIYEMCHOMA MTOTO MKONO NA KUMLISHA KINYESI, ASWEKWA JELA MAISHA

Wilvina Mukandala (24) anayetuhumiwa kumnyanyasa mtoto wa
dada yake aitwae Aneth Johannes (3) kwa kumfungia ndani na kumchoma kwa maji ya
moto mtoto huyo kisha kukatwa mkono hospitali, amehukumiwa kifungo cha maisha
jela.Pichani kushoto ndiye mtuhumiwa mwenyewe akisomewa hukumu, kulia juu ni
mtoto Aneth baada ya kuunguzwa, chini kushoto ni Aneth baada ya kukatwa mkono.
Wednesday, November 28, 2012
M23 sasa waondoka Goma
Tuesday, October 2, 2012
MAHABA NI SANAA INAYOJITEGEMEA!
je ulikutana
wapi na mpenzi wako kwa mara ya kwanza?
hili ni jambo kubwa na la msingi! katika maisha yako ya kimapenzi na hata kwa
kujiwekea kumbukumbu!
inawezekana
mmekutana katika mazingira ambayo yanweza kukufanya ujisikie aibu ama udhalili
fulani hivi, labda bar, msibani, kituo cha basi, kazini kwako, kwenye movie
mloigiza pamoja,harusini ama kwingineko.
kwangu mimi
haijalishi , ninachokusihi ni kusahau kumbukumbu mbaya akilini mwako na
kuichukua hiyo kama historia na kuifanyia kazi na kulidumisha penzi lako kadiri
unavyojaaliwa na changanya na kiasi cha ubunifu kidogo mambo yatakua mswano au
mazuri.
Tuesday, April 24, 2012
Waandamana Nusu Uchi Kulalamikia Polisi
Wanawake Uganda
Kundi la wanawake nchini Uganda wamevua nguo, nusu uchi
kulalamikia kitendo cha polisi wa Uganda anayedaiwa kumdhalilisha kingono
mwanasiasa wa upinzani. Kanda ya video imeonyesha polisi akimtomasatomasa
matiti Bi Ingrid Turinawe wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change
(FDC) baadaya kumkamata kuzuia maandamano ya wiki jana.
Naibu kamishina wa polisi Andrew Kaweesa ameomba radhi na kuahidi kufanya
uchunguzi kutokana na tukio hilo. Tangu uchaguzi mkuu mwaka 2011 ambapo rais
Yoweri Museveni alishinda Uganda imeshuhudia maandamano ya upinzani ambapo
wafuasi wengi wameishia celi za polisi.
Tukio hilo lilisababisha kuwe na ghadhabu ya umma ambapo pia lawama
zilitanda kupinga kukamatwa kwa Bi Turinawe ambaye ni kiongozi wa tawi la
wanawake katika chama cha FDC kinachoongozwa na Kizza Besigye.
Mwandishi wa BBC Siraj Kalyango amesema wanawake hao waliandamana hadi kituo
cha polisi wakiwa vifua wazi na kupeperusha mabango yaliokuwa na
maandishi,''utahisi vipi ikiwa sehemu zako nyeti zitafinywa''.Wanawake sita
walikamatwa baada ya kukataa kufunika vifua vyao, lakini wakaachiwa huru bila
masharti yeyote.
Subscribe to:
Posts (Atom)


