je ulikutana
wapi na mpenzi wako kwa mara ya kwanza?
hili ni jambo kubwa na la msingi! katika maisha yako ya kimapenzi na hata kwa
kujiwekea kumbukumbu!
inawezekana
mmekutana katika mazingira ambayo yanweza kukufanya ujisikie aibu ama udhalili
fulani hivi, labda bar, msibani, kituo cha basi, kazini kwako, kwenye movie
mloigiza pamoja,harusini ama kwingineko.
kwangu mimi
haijalishi , ninachokusihi ni kusahau kumbukumbu mbaya akilini mwako na
kuichukua hiyo kama historia na kuifanyia kazi na kulidumisha penzi lako kadiri
unavyojaaliwa na changanya na kiasi cha ubunifu kidogo mambo yatakua mswano au
mazuri.
namna ya
kudumisha ni namna ya wewe utakavyo lithamini penzi lako na hii itakufanya wewe
uonekane mpya kila siku kwa mpenzi wako, na valentain haitakua mara moja kwa mwaka katika maisha yenu ya
kimapenzi bali kila iitwapo leo!
Prince Williams na Kate Middleton's
mpende na
kumuenzi mpenzio kwa kumpa ama kumbatiza majina mazuri mazuri ama kutokana na
kilema chake cha asili pengine kama ana gubu na maneno maneno yasiyokwisha na
amri za hapa na pale sana basi mwite kamanda! ama vyovyote uwezavyo!
pia kabla
mpenzio hajalala ama kupanda kitandani basi fanya kaubunifu kwa kutupiamo
petals, unanunua ua waridi ama roses kama wenyewe waliitavyo na kulinyambua na
kisha unatupiamo kitanda kizima na kisha unarudishia bed cover kisha weka maua
ya asmini chumbani yatatoa harufu nzuri isiyokera na kisha unaendelea na
hamsini zako.
mpenzio
atakapoingia chumbani na kukutana na riha hiyo ataifurahia na atachanganyikiwa
zaidi kwa petals atakazokutana nazo chini ya bedcover! utakua ume mu win na
atakua wko maishani hakuna haja ya kumuendea kwa mganga wala nini!
Mahaba ni kuya tengeneza
mahaba ni
ubunifu kila uchao na wala usichoke! kila la kheri buni kivyako leo kisha
nishirikisha mafanikio yako!


No comments:
Post a Comment